
Kuhusu FETA Nyegezi
FETA Nyegezi ni kampasi ya pili kwa ukubwa baada ya Mbegani kwa idadi ya wanafunzi na historia ya kuanzishwa kwake. Kituo hiki (kilichokuwa kikijulikana awali kama Chuo cha Uvuvi cha Maji Baridi Nyegezi – NFFI) kilianzishwa mwaka 1967 kama kituo cha majaribio cha uchakataji samaki. Mwaka 1978, FETA Nyegezi kilibadilishwa kuwa chuo cha mafunzo na kuanza kutoa kozi ya miaka miwili ya Cheti cha Sayansi ya Uvuvi wa Jumla.
Tarehe 8 Oktoba 2011, NFFI na Mbegani Fisheries Development Centre (MFDC) viliunganishwa na kuunda Fisheries Education and Training Agency (FETA) chini ya Sheria ya Wakala wa Serikali (CAP 245) kupitia Tangazo la Serikali Na. 356.
Kwa mwaka wa masomo 2025/2026, FETA Nyegezi ina jumla ya wanafunzi 469 waliosajiliwa na imesajiliwa na kuthibitishwa na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET) kwa namba ya Usajili REG/ANE/014 kutoa kozi za Cheti na Astashahada katika Sayansi na Teknolojia ya Uvuvi, Usimamizi wa Teknolojia za Uvuvi, na Teknolojia ya Ufugaji Viumbe kwenye Maji. Aidha, kituo hiki kimeidhinishwa kutoa mafunzo ya ufundi stadi katika Ufundi Sanifu wa Majokofu na Viyoyozi yanayopelekea kupata Vyeti vya Kitaifa vya Ufundi Stadi (NVA) ngazi ya I hadi III.
Mbali na kozi ndefu zilizotajwa, FETA Nyegezi pia hutoa kozi fupi katika teknolojia ya uvuvi na ufugaji viumbe maji, hasa kwa jamii zinazozunguka Ukanda wa Ziwa Viktoria. Kozi zote zinafuata mfumo wa mafunzo unaozingatia umahiri (CBET), ulioundwa kuhakikisha kuwa mwanafunzi anapata stadi zinazohitajika na zinazoweza kutumika kwa ufasaha katika maeneo husika ya kazi pamoja na kuwaandaa wahitimu kujiajiri.
Kozi zinazopatikana katika Kampasi yetu ya Nyegezi.
Kozi Ndefu.
- Ufugaji Viumbe kwenye Maji
- Sayansi na Teknolojia ya Uvuvi
- Menejimenti ya Teknolojia ya Uvuvi
Kozi Fupi.
- Usimamizi wa Ubora, Usafi wa Viwandani na Usafi wa Mazingira
- Ukusanyaji na Uhifadhi wa Samaki
- Ujenzi wa Vyombo vya Kuhifadhia Vyenye Insulation
- Uchakataji wa Samaki wa Kiwandani
- Ufundi wa Injini Ndogo za Majini
- Teknolojia ya Nyavu na Usimamizi wa Vyombo vya Uvuvi
- Uendeshaji wa Staha na Utaalamu wa Baharini
- Uendeshaji, Matengenezo na Ukarabati wa Injini Ndogo za Nje
- Kozi Maalum kwa Wanawake katika Uvuvi
- Kozi Maalum kwa Wavuvi Wadogo
- Usimamizi Shirikishi wa Uvuvi
- Ufugaji Samaki
- Kuogelea na Uokoaji
- Mafunzo ya BMU juu ya Usimamizi wa Rasilimali Asilia
- Kozi Maalum Zinazotolewa kulingana na Mahitaji ya Mteja
Mahali Kampasi Inapopatikana
Kampasi ya Nyegezi ipo kilomita 10 kusini mwa Jiji la Mwanza, kandokando ya Ziwa Viktoria, mwishoni mwa Ghuba ya Nyegezi katika Halmashauri ya Nyamagana. Ziwa Viktoria ni moja ya maziwa makubwa barani Afrika na ni ziwa la pili kwa ukubwa duniani lenye maji baridi.
- Mratibu wa Mafunzo : Rehema Mmbaga,0768945654, rehema.mbaga@feta.ac.tz
- Mawasiliano ya Ofisi ya Udahili: 0760187242, admission.nyegezi@feta.ac.tz
- Mawasiliano ya Ofisi ya Mitihani: 0626811025, jackson.latyankira@feta.ac.tz
- Meneja wa Kampasi: Peter Masumbuko, 0767 303 847, peter.masumbuko@feta.ac.tz
- S. L. P 1213 Mtaa wa Sweya,Nyamagana, Mwanza
- Barua Pepe: nyegezi@feta.ac.tz